Wednesday, December 30, 2015

Mikutano ya Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi Oakland, California Dec. 19, 2015

Katika ziara ya Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi ya Oakland, California alikutana na wafanyabiashara katika sekta ya utalii wanaopeleka watalii Tanzania katika kampuni zao. Mhe. Balozi aliongea nao kujua changamoto wanazopata katika kupeleka watalii Tanzania, kwaajili ya kutengeneza mkakati wa kuongeza idadi ya watalii wanaoenda huko. Baada ya maongezi yao, Mhe. Balozi aliwaahidi kufuatilia mazungmzo yao na kuendelea kushirikiana katika mpango wa kuongeza idadi ya watalii. Baada ya mkutano huo Mhe. Balozi alitembelea ofisi ya Hon. Consul Bw. Ahmed Issa. 

Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi pamoja na Hon. Consul Bw. Ahmed Issa na Wafanyabiashara wa Utalii na Wadau mbalimbali wa Elimu 


Bw. Bill Roberson wa INCA, Perry Roberson wa Blue Odyssey Tours, Brenda Ross wa Sister City na Bw. Alan Feldstein wa Infinite Safari Adventures


Honurary Consul wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, California Bw. Ahmed Issa

Tuesday, December 29, 2015

End of the Year Message of H.E Ambassador Wilson Masilingi to the Tanzanians living in the United States.



 
H.E Ambassador Wilson Masilingi delivered his end of year message which called Tanzanians living in the United States of America to strengthen their cooperation and continue to be good Ambassadors of the United Republic of Tanzania to the United States of America. He also highlighted various activities that, the government of the United Republic of Tanzania through the Embassy in the United States is implementing in realization of the Economic Diplomacy. Ambassador’s message reiterated all Tanzanians in the United to engage in various economic and social initiatives so as to contribute to the country socio-economic development. He further assured the Tanzania Diaspora of the Embassy cooperation and readiness to collaborate in any initiative of interest to the people of Tanzania and the Country in General.

Thursday, December 3, 2015

MHE. BALOZI WILSON MASILINGI AKUTANA NA MHE. BALOZI HUNAINAH ALMUGHEIRY WA OMAN WASHINGTON DC



Mhe. Wilson Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani akikaribishwa ofisini kwa Mhe. Balozi Hunaina Almugheiry, Balozi wa Oman nchini Marekani.

Mheshimiwa Wilson Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani alimtembelea Mhe. Hunainah AlMugheiry, Balozi wa Oman nchini Marekani, ofisini kwake Washington DC leo Alhamisi Desemba 3,2015. Katika mazungumzo Mhe. Balozi Masilingi aliambatana na Bw. Suleiman Ahmed Saleh, Afisa wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC.

Mazungumzo kati ya Mhe. Balozi Masilingi na Mhe. Mugheiry yalilenga katika kuimarisha mahusiano kati ya nchi hizo mbili zenye mahusiano ya kidugu. Mhe. Balozi Mugheiry alifurahishwa na kuonana na Mhe. Masilingi na kubainisha kwamba Oman na Tanzania zina mahusiano ya kidamu na hivyo nchi hizo hazina budi kudumisha mahusiano hayo ya kihistoria. Mhe. Mugheiry alimweleza Balozi Masilingi kwamba amefarijika uchaguzi wa Tanzania ulikwisha salama na Tanzania kumpata mrithi wa Rais mpya Mhe. John Pombe Magufuli kufuatia kumaliza muda wake Rais aliyepita Mhe. Jakaya Kikwete.Aliongeza kwa kusema kwamba Oman na Tanzania zimekuwa na mashirikiano ya kiuchumi,kibiashara na kielimu na anaamini kwamba ujenzi wa bandari ya Bagamoyo na fursa za masomo ya juu zinazotolewa na Serikali ya Oman kwa wanafunzi wa Tanzania Bara na Visiwani ni vielelezo vya mahusiano hayo.

Kwa upande wake Mhe. Balozi Masilingi alifarijika sana kumsikia Mhe. Balozi Hunainah wa Oman akimwambia kwamba alizaliwa Dar-es-Salaam, Tanzania, na familia yake ina mizizi visiwani Zanzibar pia. Alimshukuru Balozi Hunainah kwa kumkaribisha ofisini kwake na kufahamiana naye na kuahidi kufanya naye kazi kwa karibu katika kuendeleza mahusiano baina ya nchi zao zenye mahusiano ya asili.

Mhe. Wilson Masilingi katika picha ya kumbukumbu na Mhe. Hunainah Almugheiry

TANGAZO


UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, 
WASHINGTON, D.C.
 
TANGAZO

Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi anawakaribisha Watanzania wote na Wamarekani wenye asili ya Kitanzania kwenye mkutano mfupi wa kufahamiana utakaofanyika tarehe 12 Desemba, 2015.

Mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa Tabeer uliopo 1401 University Boulevard, Hyattsville Maryland 20783, kuanzia saa tisa hadi saa kumi na moja jioni (3:00pm – 5:00pm).

Wote mnakaribishwa, na tafadhali zingatieni muda.

Tuesday, December 1, 2015

MHE. BALOZI WILSON M. MASILINGI AKUTANA NA BI. CATHY BYRNE, MKURUGENZI MWANDAMIZI WA MASUALA YA AFRIKA, IKULU YA MAREKANI (WHITE HOUSE) TAREHE 30 NOVEMBA 2015

Mhe. Balozi Masilingi alitembelea ofisi ya Bi. Cathy Byrne, Mkurugenzi Mwandamizi wa masuala ya Afrika katika Ikulu ya Marekani (White House). Wakati wa mazungmzo yao, Bi. Cathy Byrne alimueleza Mhe. Balozi Masilingi kuwa Serikali ya Marekani inaridhishwa na mahusiano mazuri yaliyopo baina yake na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Marekani. Aidha alieleza kuwa Serikali ya Marekani inaridhishwa na hatua mbalimbali zinachukuliwa na serikali ya Tanzania, katika kuwaletea wananchi wake maendeleo.

Mhe. Balozi Masilingi amemhakikishia mwenyeji wake kuwa ataendeleza mashirikiano mazuri sana yaliyopo kati ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Marekani kwa njia ya diplomasia ya uchumi yenye lengo la kuhamasisha biashara na uwekezaji nchini Tanzania.


Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi akiagana na Bi. Cathy Byrne mara baada ya kumaliza mazungmzo yao.

MHE. BALOZI WILSON M. MASILINGI, BALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGMZO NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA DUNIA, KANDA YA AFRIKA, BW. LOUIS RENE PETER LAROSE. TAREHE 30.11.2015 KATIKA OFISI YA BENKI YA DUNIA

Mhe. Wilson M. Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, akifuatana na Bw. Paul Mwafongo alihudhuria mkutano na Bw. Louis Rene Peter Larose, Mkurugenzi Mtendaji, Benki ya Dunia, Kundi la Nchi za Afrika. Wengine waliohudhuria ni pamoja na Bw. Andrew Ndaamunhu Bvumbe, Mkurugenzi Mtendaji Mbadala Benki ya Dunia, Kanda ya Afrika, na Bw. WilsonToninga Banda, Mshauri, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji.

Shabaha ya Mkutano ilikuwa ni kufuatilia mazungumzo yaliyofanyika Lima, Peru kuhusu kuimarisha ushirikiano kwa maslahi ya Afrika. Mhe. Balozi Masilingi alishukuru Benki ya Dunia kwa ushirikiano mzuri uliopo na kwa misaada na mikopo wanayotoa kuunga mkono juhudi za kujenga uchumi na kufanikisha mipango ya maendeleo kwa manufaa ya Watanzania wote. Aidha aliwahakikishia ushirikiano muda wote atakapokuwa katika kutekeleza wajibu wake wa kazi kwa maslahi ya Taifa. Mkurugenzi Mtendaji Benki ya Dunia, Kanda la Afrika, Bw. Louis Larose, alieleza kwa upande wake kuridhirishwa kwake na ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Benki ya Dunia. Aidha Bw. Larose aliipongeza Tanzania kwa kufanikisha Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba , 2015 kwamba ulikuwa huru na wa haki. Pia, alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John P. Magufuli kwa ushindi na kwa juhudi zake katika kuangalia udhibiti wa ukusanyaji wa mapato ya serikali na kuziba mianya ya uvujaji wa mapatao ili zipatikane fedha kwa ajili ya kusukuma maendeleo ya Watanzania.

Mkurugenzi Mtendaji aliahidi kwamba Benki ya Dunia iko tayari kutoa msaada wowote wa haraka utakaohitajika na kuombwa na Serikali ya Tanzania ili kufanikisha mpango wa kukusanya mapato ya ndani kwa ajili ya kutekeleza program za maendeleo na huduma za serikali.

Bw. Larose, alimdokeza Mhe. Balozi kwamba Benki ya Dunia itaandaa siku maalumu mjini Washington, D.C. kwa ajili ya kuitangaza Tanzania na vivutio vyake nchini Marekani na kuomba kwamba Benki ya Dunia itamwalika Mhe. Balozi kuzindua siku hiyo. Akijibu hoja hiyo Mhe. Balozi alikubali mwaliko huo.


Mhe. Wilson M. Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, (Katikati) akiwa na Bw. Louis Rene Peter Larose, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia, Kanda ya Afrika (mkono wa kushoto wa Balozi) Wengine Bw. Paul Mwafongo, Mwambata Uchumi wa Ubalozi (wa kwanza kushoto), Bw. Andrew Ndaamunhu, Mkurugenzi Mtendaji Mbadala, Kanda ya Afrika (wapili kushoto) na Bw. Wilson Toninga Banda, Mshauri, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (wa kwanza kulia)


Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi (kushoto) katika picha ya pamoja na Bw. Louis Rene Peter Larose, Mkurugenzi Mtendaji, Kanda ya Afrika (kushoto), Ofisi za Benki ya Dunia


Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi (kushoto) katika mazungumzo ofisini kwa mwenyeji wake Bw. Louis Rene Peter Larose.

Tuesday, November 3, 2015

COMPETITION: Carnegie African Diaspora Fellowship Program



Applications are now being accepted through
December 8, 2015
for the Fall 2015 competition of the Carnegie African Diaspora Fellowship Program.

·         Public and private higher education institutions in Ghana, Nigeria, Kenya, Tanzania, South Africa and Uganda, accredited by the national agency in their country, can submit a project request online to host a scholar.
·         Scholars born in Africa, who live in the United States or Canada and work in an accredited college or university in either of those two countries, can apply online to be placed on a roster of available candidates for a fellowship. Scholars must hold a terminal degree in their field and may hold any academic rank.

Links to the African host institution project request application, scholar roster application and guidelines are all posted on the program website, http://www.iie.org/en/Programs/Carnegie-African-Diaspora-Fellows-Program/How-to-Apply.
Selection decisions for the first round will be in March 2016; project visit can begin as early as May 2016.

Activities: African host institutions can request that the scholar participate in mutually beneficial projects in curriculum co-development, research collaboration and/or graduate student mentoring and training. The CADFP Advisory Council seeks applications for innovative projects, and specifically encourages projects that involve collaboration among multiple institutions or from groups of faculty who are addressing related topics.  As a way of solidifying links that have already been developed between host institutions and visiting scholars, the council also plans to award some fellowships to faculty members who are alumni from the first two years of the program
Process:  Prospective African host institutions and fellows (scholars) can cooperate in designing a project that the institution submits. An institution may, but is not required to, name a proposed scholar in a project request. Both the proposed scholar and the project request are subject to evaluation by a review committee and approval by the program Advisory Council.
Scholars submit their information online for the roster. The Institute of International Education (IIE) maintains and searches the roster for one or more possible matches, according to the discipline specializations, expertise, activities and objectives described in a project request.
Fellowship:  Projects can be conducted in the African host country for 14-90 days. For the fellowship, the African Diaspora Fellow will receive:
·         $200/day stipend
·         visa costs
·         limited health insurance coverage
·         round-trip international air travel and ground transportation costs to and from home and the U.S./Canadian airport.

IIE manages the fellowships and payments to fellows. Host institutions are encouraged to provide cost-share for the fellow’s meals, lodging and in-country transportation during the project.
Please contact:
Jeremy Coats
Program Officer
Carnegie African Diaspora Fellowship Program
Scholar Exchanges Division
Institute of International Education (IIE)
Tel: 202.686.6231; Fax: 202.686.4029
Email
: africandiaspora@iie.org

Tuesday, October 20, 2015

PERMANENT SECRETARY OF THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION H.E. AMBASSADOR LIBERATA MULAMULA VISITS THE EMBASSY OF TANZANIA, WASHINGTON DC.

H.E. Permanent Secretary Ambassador Liberata Mulamula greets the staff at the Embassy of Tanzania, Washington DC
 H.E. Ambassador Mulamula signs the guest book at the Tanzania House

 H.E. Ambassador Mulamula with the Head of Chancery Mrs. Swahiba H. Mndeme.
 
H.E. Ambassador Mulamula having a meeting with staff of the
Embassy of Tanzania, Washington D.C
H.E.Ambassador Mulamula with officers of the Embassy of Tanzania
H.E. Ambassador Mulamula in a picture with some staff at the
Embassy of Tanzania, Washington DC.

MS. BAHATI MURIGA TANZANIAN FARMER HONORED BY OXFAM IN A RECEPTOPN AT THE EMBASSY OF TANZANIA IN WASHINGTON DC

On Thursday October 9th 2015, the Embassy of Tanzania in Washington DC hosted a reception of guests, sponsored by Oxfam, to highlight their Female Food Hero initiative. Ms. Bahati Muriga was a guest speaker who spoke concerning her work as a farmer, also known for winning the Swahili reality television series “Mama Shujaa wa Chakula”. Ms. Muriga lives in the Mwanza region of northern Tanzania and shorty after becoming a widow she began to look for ways to support her two children while working as head of a primary school she continued to take on more of her husband’s farming. The extra income from her farming activities enabled her to provide education for her children and take care of many other family needs.
 
The Embassy of Tanzania hosted the event for the Female Food Hero who came to DC from Tanzania. The Oxfam event comes in advance of World Food Day (October 16th) and is part of Oxfam America’s overall activities around World Food Day which includes high level presence in Iowa at the World Food Prize where our Female Food Hero will be a featured speaker/guest at several events.  Ms. Muriga will also travel to Des Moines, Iowa to take part in World Food Prize events.
See also:

 Ms. Bahati Muriga speaking to guests at the reception
 
 Ms. Bahati Muruga with Embassy officer Mr. Suleiman Saleh.
 
Mayor Mlima of the Embassy with Ariel from Fair Trade America

Tuesday, August 25, 2015

H.E. Ambassador Wilson Masilingi arrives at the Embassy of Tanzania in Washington DC

 
His Excellency Ambassador Wilson Masilingi as he greets the staff of the Embassy of Tanzania in Washington DC
H.E. Ambassador Wilson Masilingi signing into his office at the Tanzania House  
H.E. Ambassador Wilson Masilingi in a brief meeting with the Defense Attaché Col. Adolph Mutta and Consular Officer Mr. Abbas Missana.